Bodi moja nchini Afrika Kusini imeamua kuwa misaada ya kifedha kwa wanafunzi wa vyuo vikuu walio mabikra inakiuka sheria na inafaa kufutiliwa mbali. Baraza la mji wa KwaZulu-Natal lilianzisha fedha hizo ili kupunguza viwango vya ukimwi na mimba za utotoni. Lakini tume ya usawa wa jinsia imesema kuwa msaada huo unaowalenga wasichana mabikra pekee unabagua. Mpango huo ulizua hisia kali ulipoanzishwa mapema mwaka huu. Katika uamuzi wake baada ya makundi ya haki za kibinaadamu kuwasilisha lalama zao,Tume hiyo ilisema: Unakiuka sheria kuhusiana na heshima, usawa na ubaguzi.
No comments:
Post a Comment